Wednesday, May 25, 2016

JUVENTUS YATAKA KUMNG'OA MASCHERANO CAMP NOU.

KIUNGO mahiri wa Barcelona, Javier Mascherano anadaiwa kukubali dili la kujiunga na mabingwa wa Serie A Juventus. Taarifa zinadai kuwa nyota huyo wa kimataifa wa Argentina amefanya mazungumzo na Juventus na anajiandaa kuhamia jijini Turin kiangazi hiki. Mpaka sasa inadaiwa kuwa hakuna makubaliano yeyote kati ya Barcelona na Juventus na mabingwa hao wa Hispania wanahisiwa kutokuwa na mpango wowote wa kumuachia kiungo huyo mwenye umri wa miaka 31. Mascherano alijiunga na Barcelona mwaka 2010 akitokea Liverpool, na kufanikiwa kushinda mataji manne ya La Liga na mawili ya Ligi ya Mabingwa Ulaya akiwa Camp Nou.

No comments:

Post a Comment