Tuesday, May 31, 2016

MARCO REUS ATEMWA KIKOSI CHA UJERUMANI.

KOCHA wa timu ya taifa ya Ujerumani, Joachim Low amemuacha mshambuliaji wa Borussia Dortmund Marco Reus katika kikosi chake cha mwisho cha wachezaji 23 kwa ajili ya michuano ya Euro 2016. Low alitangaza kikosi chake huku mbali na kumuacha Reus lakini pia amewaacha Karim Bellarabi na Julian Brandt wa Bayer Leverkusen na Sebastian Rudy wa Hoffenheim. Nyota hao wanne sasa wanatarajiwa kuondoka katika kambi ya timu hiyo huo Uswisi. Ujerumani itacheza mechi yake ya mwisho ya kujipima nguvu dhidi ya Hungary kabla ya kucheza mechi yao ya ufunguzi wa michuano ya Euro 2016 dhidi ya Ukraine.

Kikosi kamili ni
Makipa: Manuel Neuer (Bayern Munich), Bernd Leno (Bayer Leverkusen), Marc-Andre ter Stegen (Barcelona)

Mabeki: Jerome Boateng (Bayern Munich), Emre Can (Liverpool), Jonas Hector (Cologne), Benedikt Howedes (Schalke), Mats Hummels (Borussia Dortmund), Shkodran Mustafi (Valencia), Antonio Rudiger (Roma)

Viungo: Julian Draxler (Wolfsburg), Mario Gotze (Bayern Munich), Sami Khedira (Juventus), Joshua Kimmich (Bayern Munich), Toni Kroos (Real Madrid), Mesut Ozil (Arsenal), Leroy Sane (Schalke), Bastian Schweinsteiger (Manchester United), Julian Weigl (Borussia Dortmund)

Washambuliaji: Mario Gomez (Besiktas), Thomas Muller (Bayern Munich), Lukas Podolski (Galatasaray), Andre Schurrle (Wolfsburg)

No comments:

Post a Comment