Tuesday, May 31, 2016

SENDEROS AACHWA TIMU YA TAIFA.

BEKI wa zamani wa Arsenal, Philippe Senderos ambaye amekuwa akihangaika kurejea katika kiwango chake katika misimu ya karibuni, ameachwa katika kikosi cha timu ya taifa ya Uswisi kwa ajili ya michuano ya Euro 2016. Senderos ambaye ametumia muda mwingi msimu uliopita akiwa na timu yake ya nyumbani ya Grasshopper Zurich, alishindw akuonyesha uwezo wake wakati Uswisi walipotandikwa mabao 2-1 na Ubelgiji katika mchezo wa kirafiki wa kujipima nguvu. Kocha wan chi hiyo Vladimir Petkovic ameamua kumuacha beki huyo mwenye umri wa miaka 31 pamoja an wasiwasi uliopo katika safu ya ulinzi kutokana na Timm Klose na Johan Djourou kuwa nje kutokana na majeruhi. Beki wa Udenese Silvan Widmer na kiungo wa basel Luca Zuffi ambye ameonyesha uwezo mkubwa msimu huu pia wamekatwa katika kikosi hicho. Uswisi inatarajiw akucheza na Moldova katika mechi yake ya mwisho ya kujipima nguvu Ijumaa hii kabla ya kuvaana na Albania, Romania na wenyeji Ufaransa katika kundi A.

Kikosi Kamili ni
Makipa: Yann Sommer (Borussia Monchengladbach), Roman Burki (Borussia Dortmund), Marwin Hitz (Augsburg)

Mabeki: Stephan Lichtsteiner (Juventus), Nico Elvedi (Borussia Monchengladbach), Michael Lang (Basel), Johan Djourou (Hamburg), Steve von Bergen (Young Boys), Fabian Schar (Hoffenheim), Francois Moubandje (Toulouse), Ricardo Rodriguez (Wolfsburg)

Viungo: Valon Behrami (Watford), Blerim Dzemaili (Genoa), Gelson Fernandes (Rennes), Fabian Frei (Mainz), Granit Xhaka (Arsenal), Xherdan Shaqiri (Stoke City), Renato Steffen (Basel), Denis Zakaria (Young Boys)

Washambuliaji: Breel Embolo (Basel), Haris Seferovic (Eintracht Frankfurt), Admir Mehmedi (Bayer Leverkusen), Eren Derdiyok (Kasimpasa), Shani Tarashaj (Everton)

No comments:

Post a Comment