Tuesday, May 31, 2016

CURRY AIPELEKA WARRIORS FAINALI YA NBA.

ALAMA 36 zilizofungwa na nyota Stephen Curry ziliiwezesha Golden State Warriors kuibuka na ushindi wa vikapu 96-88 dhidi ya Oklahoma City Thunder na kuwawezesha kutinga fainali ya Ligi ya Mpira wa Kikapu nchini Marekani maarufu kama NBA. Warriors walikuwa nyuma kwa alama 13 wakati wa kipindi cha kwanza lakini walipambana katika na kurejea mchezoni katika robo ya mwisho katika mchezo huo. Ushindi wa jumla wa michezo 4-3 unaifanya Warriors kuwa timu ya 10 ambayo imepambana kutoka kufungwa kwa 3-1 na kuibuka washindi katika hatua hiyo ya mtoano. Mabingwa hao watetezi wa NBA sasa watakabiliaa kwa mara nyingine na Cleveland Cavaliers wakiwa na nyota wao LeBron James katika hatua ya fainali ambayo itakuwa na michezo saba. Warriors wataivaa Cavaliers katika mchezo wa kwanza utakaofanyika Alhamisi hii huku wakiwa na matumaini ya kuibuka mabingwa kama walivyofanya mwaka jana waliposhinda kwa michezo 4-2.

No comments:

Post a Comment