Tuesday, May 31, 2016

NAVAS KUIKOSA COPA AMERICA.

GOLIKIPA wa kimataifa wa Costa Rica na klabu ya Real Madrid, Keylor Navas anatarajiwa kuikosa michuano maalumu ya Copa Amerika kwasababu ya majeruhi ya kisigino. Majeruhi hayo aliyopata katika mguu wake wa kushoto yalimfanya kuukosa michezo muhimu ya Madrid mwishoni mwa msimu. Jana Shirikisho la Soka la Costa Rica-FEDEFUTBOL, lilithibitisha taarifa za kumuondoa nyota huyo na nafasi yake kuchukuliwa na kipa Deportivo Saprissa Danny Carvajal. Navas anatarajiwa kutafuta mtaalamu atakayetibu tatizo lake hilo ambalo pia lilimkosesha michuano ya michuano ya Kombe la CONCACAF Gold mwaka jana. Kukosekana kwa Navas na mshambuliaji nyota Ariel Rodriquez ni pigo kubwa kwa Costa Rica ambao wamepangwa katika kundi A sambamba na Marekani, Paraguay na Colombia.

No comments:

Post a Comment