Tuesday, May 31, 2016

ARGENTINA YATISHIA KUJITOA COPA AMERICA.

CHAMA cha Soka cha Argentina-AFA kimetishia kujitoa katika michuano maalumu ya Copa America baada ya kuituhumu serikali ya nchi yao kwa kuwaingilia. Argentina ni moja ya timu zinazopewa naafsi ya kufanya vizuri katika michuano hiyo itakayofanyika nchini Marekani huku wakitarajiwa kucheza mechi yao ya kwanza dhidi ya mabingwa watetezi Chile huko Santa Clara, California Juni 7 mwaka huu. Hata hivyo, AFA wamezusha wasiwasi wa kutokuwepo kwa mchezo huo baada ya serikali ya Argentina kusimamisha uchaguzi wa chama hicho ambao ulikuwa ufanyike Juni 30 na kuteua tume maalumu ya kuchunguza tuhuma za ubadhilifu wa mapato ya luninga. Katibu Mkuu wa AFA, Damian Dupiellet amesema mkutano wa dharura wa bodi ndio utakaoamua kama timu yao ya taifa itashiriki michuano hiyo au itarudishwa nyumbani kutoka katika kambi yao huko Marekani.

No comments:

Post a Comment