Tuesday, May 31, 2016

KESI YA MESSI YAANZA KUSIKILIZWA.

KESI ya ukwepaji kodi dhidi ya mshambuliaji nyota wa kimataifa wa Argentina, Lionel Messi imeanza kusikilizwa jijini Barcelona leo. Messi na baba yake wameshitakiwa kwa makosa matatu ya ukwepaji kodi yenye thamani ya euro milioni 4.1 kuanzia mwaka 2007 mpaka 2009. Nyota huyo wa Barcelona anatarajiwa kupanda kizimbani mwenyewe kutoa ushahidi wake Alhamisi hii, ikiwa ni siku nne kabla ya mechi ya ufunguzi ya michuano ya Copa America dhidi ya mabingwa watetezi Chile. Wakili wa Messi, Enrique Bacigalupo ndio aliyemwakilisha nyota huyo leo katika Mahakama hiyo ya Eighth.

No comments:

Post a Comment