Monday, May 30, 2016

RASHFORD APIGWA MIAKA MINNE MINGINE OLD TRAFFORD.

MSHAMBULIAJI nyota wa Manchester United, Marcus Rashford mwenye umri wa miaka 18 amesaini mkataba mpya ambao utamuweka Old Trafford mpaka Juni mwaka 2020. Chipukizi huyo alifunga mabao mawili katika mechi yake ya kwanza katika kikosi cha wakubwa dhidi ya Midtjlland Februari mwaka huu na kumaliza akiwa amefunga mabao nane katika mechi 18 alizocheza. Kiwango hicho kizuri alichokionyesha kilimfanya kuteuliw akatika kikosi cha Uingereza na kufunga bao lake la kwanza katika mchezo wa kirafiki dhidi ya Australia Ijumaa iliyopita. Akihojiwa Rashford amesema anajisikia furaha kwa kupewa nafasi ya kuonyesha uwezo wake na kuahidi wa mashabiki wa United kuwa wategemee mambo mazuri kutoka kwake.

No comments:

Post a Comment