Friday, May 27, 2016

WAKALA WA ALVES AKANUSHA TAARIFA ZA KWENDA JUVENTUS.

WAKALA wa Dani Alves amekanusha taarifa kuwa mteja wake amesaini mkataba wa awali na Juventus lakini amekiri mabingwa wa Italia na klabu zingine zinamuwania mchezaji huyo. Vyombo vya habari nchini Hispania viliripoti jana kuwa beki huyo wa Barcelona anatarajiwa kuondoka baada ya kutimukia timu hiyo kwa miaka nane na kwenda Turin kwa mkataba wa miaka mitatu. Hata hivyo, wakala wake ambaye pia amewahi kuwa mke wake, Dinorah Santa Ana da Silva alikanusha taarifa hizo akidai hazina ukweli wowote. Dinorah aliongeza kuwa hakuna klabu yeyote Alves aliyosaini hivi sasa kwani amehamishia nguvu zake zote katika timu ya taifa ya Brazil ambayo inakabiliwa na michuno ya Copa America mapema mwezi ujao. Wakala huyo aliendelea kudai kuwa ni kweli amekutana na Juventus lakini sio wao peke yao kwani amekutana pia na klabu zingine lakini hakuna dili lolote lililoafikiwa mpaka sasa.

No comments:

Post a Comment