Friday, May 27, 2016

KAKA AITWA BRAZIL.

MSHAMBULIAJI wa Orlando City, Kaka ameitwa katika katika kikosi cha timu ya taifa ya Brazil kwa ajili ya michuano ya Copa America akichukua nafasi ya Douglas Costa. Costa mwenye umri wa miaka 25, amepata majeruhi misuli ambayo yatamfanya kukosa michuano hiyo maalumu ya kuadhimisha miaka 100 toka kuanzishwa kwake. Kaka mwenye umri wa miaka 34 ameichezea Brazil mechi 91 na kufunga mabao 29 katika kikosi cha Brazil. Costa alikuwa sehemu ya kikosi cha Bayern Munich ambacho kimeshinda taji la Bundesliga na Kombe la Ujerumani katika msimu wa mwisho wa Pep Guardiola na timu hiyo. Brazil itafungua pazia la Copa America kwa kucheza na Ecuador katika Uwanja wa Rose Bowl huko Pasadena, California Juni 4 mwaka huu huku mechi zao nyingine mbili za kundi B zitakuwa dhidi ya Haiti na Peru.

No comments:

Post a Comment