Friday, May 27, 2016

RONALDO AWANANGA BARCELONA NA MATAJI YAO MAWILI.


MSHAMBULIAJI nyota wa Real Madrid, Cristiano Ronaldo amesema kushinda taji la Ligi ya Mabingwa Ulaya kutakuwa na tahmani zaidi ya mataji mawili ambayo Barcelona wameshinda. Nyota huyo mwenye umri wa miaka 31 alikuwa akisumbuliwa na majeruhi katika wiki za karibuni na kumfanya kukosa nusu fainali ya mkondo wa kwanza ya Ligi ya Mabingwa Ulaya dhidi ya Manchester City. Hata hivyo juzi aliwaondoa hofu mashabiki wa timu hiyo akidai kuwa atakuwa fiti kwa asilimia 100 kwa ajili ya fainali hiyo dhidi ya mahasimu wao Atletico Madrid. Akihojiwa Ronaldo amesema kama wakishinda taji la Ligi ya Mabingwa itakuwa na thamani zaidi kuliko mataji mawili ya Barcelona waliyoshinda kwani taji la michuano hiyo liko katika ndoto za kila mchezaji. Madrid na Atletico wanakutana katika fainali tatu ambazo zimekutanisha timu za Hispania na fainali mbili baina yao.

No comments:

Post a Comment