Friday, May 27, 2016

MOURINHO RASMI UNITED.

KLABU ya Manchester United imemthibitisha rasmi Jose Mourinho kuwa meneja wao mpya baada ya kusaini mkataba wa miaka mitatu. Mourinho anachukua nafasi ya Mholanzi Louis van Gaal ambaye alitimuliwa Jumatatu, siku mbili baada ya kutwaa taji la Kombe la FA. Makamu mwenyekiti wa United, Ed Woodward amesema Mourinho ndio meneja bora katika mchezo wa soka kwasasa. Naye Mourinho mwenye umri wa miaka 53, akihojiwa amesema kuwa meneja wa klabu hiyo ni heshima kubwa kwake kwani United inajulikana na kupendwa duniani kote. Mourinho amekuwa bila kibarua toka alipotimuliwa kuinoa Chelsea Desemba mwaka jana.

No comments:

Post a Comment