Wednesday, May 25, 2016

ARSENAL YAANZA USAJILI KWA KUMNASA XHAKA.

KLABU ya Arsenal imekamilisha rasmi usajili wa Grant Xhaka kutoka Borussia Monchengladbach kwa dili lenye thamani ya paundi milioni 33.1. Nyota huyo mwenye umri wa miaka 23 aliwasili katika viwanja vya mazoezi vya klabu hiyo Ijumaa iliyopita kwa ajili ya vipimo vya afya na kumalizia hatua za mwisho za usajili wake wa miaka minne. Ujio wa Xhaka kabla ya kuanza kwa usajili kunaonyesha jinsi Arsene Wenger alivyopania kuimarisha kikosi chake ambacho kilishika nafasi ya pili katika msimamo wa Ligi Kuu msimu uliopita. Akihojiwa Xhaka amesema anajivunia kujiunga na Arsenal kwa ni moja ya klabu kubwa ambazo amekuwa akitamani siku nyingi kuzichezea. Naye Wenger akihojiwa amesema Xhaka ni mchezaji mzuri mwenye uzoefu wa michuano ya Ligi ya Mabingwa Ulaya na Bundesliga na wamekuwa wakimfuatilia kwa kipindi kirefu.

No comments:

Post a Comment