Tuesday, June 28, 2016

BAADA YA KUTUA RASMI JUVENTUS, ALVES APANIA TAJI LA CHAMPIONS LEAGUE.

BEKI wa kimataifa wa Brazil, Dani Alves amepania kushinda kupelekea taji la Ligi ya Mabingwa Ulaya Juventus baada ya kukamilisha uhamisho wake kutoka Barcelona. Nyota huyo alioyeondoka Camp Nou kwenda Turin kama mchezaji huru, amesaini mkataba wa miaka miwili jana huku kukiwa na chaguo na kuongezewa mwingine mmoja. Beki huyo wa kulia alikuwa sehemu ya kikosi cha Barcelona kilichowanyima Juventus mataji matatu kwa kuwafunga katika hatua ya fainali ya michuano ya Ligi ya Mabingwa Ulaya mwaka 2015 iliyofanyika jijini Berlin. Lakini sasa Alves ana matumaini ya kuisaidia klabu hiyo kutwaa taji lake la kwanza la Ulaya toka walipofanya hivyo msimu wa 1995-1996. Akihojiwa Alves amesema ni heshima kubwa kuwa sehemu ya kikosi hicho kwani Juventus wana ndoto kubwa na angependa kuwasaidia kuzitimiza.


No comments:

Post a Comment