Tuesday, June 28, 2016

MARADONA, RAIS WA ARGENTINA WAMUANGUKIA MESSI ABADILI UAMUZI WA KUSTAAFU.

NGULI wa soka wa Argentina, Diego Maradona amemtaka Lionel Messi kutoendelea na uamuzi wake wa kustaafu soka la kimataifa baada ya kipigo walichopata katika fainali ya michuano ya Copa America. Maradona alikakariwa na gazeti moja nchini wake akimtaka Messi abakie katika timu ya taifa kwasababu bado muda wake rasmi wa kufanya hivyo haujafika. Nguli aliongeza kuwa ana imani Messi atakwenda nchini Urusi akiwa katika kiwango cha juu ili kuwa bingwa wa dunia katika Kombe la Dunia mwaka 2018. Messi mwenye umri wa miaka 29, aliwaambia wanahabari nchini Marekani uamuzi wake wa kuamua kustaafu soka la kimataifa baada ya Argentina kuchapwa kwa changamoto ya mikwaju ya penati na Chile Jumatatu Alfajiri. Maradona ambaye amewahi kunyakuwa Kombe la Dunia mwaka 1986 akiwa na Argentina, alilaumu ukame wa mataji kwa nchi hiyo unatokana na Chama chao cha soka-AFA. Mbali na Mardona lakini pia wa rais wa Argentina, Mauricio Macri naye amemuangukia Messi akimtaka kuteungua uamuzi wake huo.

No comments:

Post a Comment