Tuesday, June 28, 2016

INIESTA APONDA KIWANGO KIBOVU CHA TIMU YAO.

KIUNGO mahiri wa kimataifa wa Hispania, Andres Iniesta amekiri uchezaji wa hovyo wa kipindi cha kwanza ndio uliowagharimu na kuepelekea kutolewa katika michuano ya Ulaya na Italia jana. Akihojiwa Iniesta amesema ni vigumu kukubali kufungwa lakini wamekubali kwasababu tatizo lilikuwa katika masuala ya kiufundi zaidi. Italia walishinda mchezo huo kwa mabao 2-0 huko Stade de France huku Giorgio Chiellini akifunga bao la kuongoza katika kipindi cha kwanza kabla ya Graziano Pelle hajafunga la ushindi katika dakika za majeruhi. Iniesta amesema anadhani walikuwa wanasubiri sana kuona kitu gani wapinzani wao watafanya na mambo kama hayo muda mwingine lazima yakugharimu. Nyota huyo aliongeza kuwa hilo ndio kosa walilofanya kipindi kwanza lakini kipindi walikuwa tofauti na walicheza zaidi kama wlaivyozoea.

No comments:

Post a Comment