Tuesday, June 28, 2016

COPA AMERICA YAMUACHA SANCHEZ NA MAJERUHI.

MSHAMBULIAJI mahiri wa kimataifa wa Chile na klabu ya Arsenal Alexis Sanchez anatarajiwa kuwa nje ya uwanja kw amuda kufuatia kuumia kifundo chake cha mguu katika mchezo wa fainali ya michuano ya Copa America dhidi ya Argentina jana. Nyota huyo alipiga picha na kuituma katika mitandao wa kijamii ikionyesha jinsi kifundo cha mkuu wake wa kushoto kilivyovimba huku picha nyingine ikionyesha bandeji gumu alilofunga. Sanchez alitwaa tuzo ya Mpira wa Dhahabu ya mchezo bora wa mashindano baada ya Chile kuichapa Argentina kwa changamoto ya mikwaju ya penati ikiw ani mara ya pili mfululizo kutwaa taji hilo. Nyota huyo alimaliza akiwa amefunga mabao matatu na kusaidia mengine mawili lakini alitolewa katika muda wa nyongeza wakati wa mchezo huo hali ambayo haikuwa ya kawaida kwa mchezaji kama yeye aliyezoea kucheza dakika zote. Akiwa hajatoa maelezo yeyote ni kwa kiasi gani alivyoumia, Sanchez aliandika katika mtandao wake kuwa anafuraha pamoja na kuumia kwake kwa ilistahili.

No comments:

Post a Comment