Tuesday, June 28, 2016

BREXIT KUCHELESHA USAJILI LIGI KUU.

WAKILI wa masuala ya michezo, Carol Couse amedai kuwa kura za kihistoria za Uingereza kujitoa katika Umoja wa Ulaya-EU Alhamisi iliyopita, kunaweza kupelekea kuchelewa kufanyika kwa usajili kwa kipindi hiki cha kiangazi. Uamuzi wa kura hizo tayari umeshaanza kuleta athari nchini Uingereza kwa kusababisha sarafu yao kuporomoka na kuzidiwa na ile ya euro. Timu zote 20 za Ligi Kuu zilikuwa zikiunga mkono kampeni ya kubakia ndani ya EU, kutokana na wasiwasi wa kupanda gharama kwa vibali vya kazi kwa wachezaji kutoka nje na kunyima uwezo wa kusajili wachezaji wapya. Dirisha la usajili limefunguliw arasmi Ijumma iliyopita kama ilivyo ada na Couse ambaye anafanya kazi katika klabu kadhaa kubwa ikiwemo Manchester United anafikiri timu za Ligi Kuu zitasubiri mpaka Agosti ili kununua wachezaji. Couse aliendelea kudai kuwa hatua hiyo itakuja ili wasubiri sarafu ya paundi itulie kwanza, hivyo kufanya klabu kufanya usajili wa haraka haraka mwishoni kukimbizana na muda.

No comments:

Post a Comment