Tuesday, June 28, 2016

HODGSON AWAJIBIKA KABLA YA KUWAJIBISHWA.

KOCHA wa timu ya taifa ya Uingereza, amejiuzulu punde kufuatia kipigo cha fedheha cha mabao 2-1 walichopata kutoka kwa timu ndogo ya Iceland katika michuano ya Ulaya inayoendelea nchini Ufaransa. Mkataba wa Hodgson ulikuwa umelizike baada ya michuano hii na kufuatia mchezo huo uliofanyika jijini Nice, aliwaambia wanahabari katika taarifa aliyoiandaa kuwa hataweza kuendelea tena kuinoa timu hiyo. Hodgson mwenye umri wa miaka 68 ambaye alichukua mikoba kutoka kwa Fabio Capello maka 2012 amesema angependa kuendelea kubakia lakini kutokana na hali ilivyo anadhani ni vyema kumpisha mtu mwingine. Kocha huyo aliendelea kudai kuwa kikosi cha Uingereza kimesheheni vijana wenye vipaji ambao wana uchu na nja ya mafanikio hivyo anadhani atakayechukua nafasi yake ataendeleza alipoachia. Mara baada ya kumaliza kusoma taarifa yake Hodgson aliondoka haraka na msemaji wa Chama cha Soka cha Uingereza-FA Ray Lewington akidai kuwa kocha huyo hatafanya mazungumzo mengine na wana habari.

No comments:

Post a Comment