Monday, June 27, 2016

MAN UNITED YAMSHIKIA BANGO POGBA, IBRAHIMOVIC NAYE ANUKIA.

KLABU ya Manchester United inadaiwa kutaka kuendelea na mpango wake wa kumrudisha tena kiungo mahiri wa kimataifa wa Ufaransa Paul Pogba. United ilimuuza Pogba akiwa mdogo kwenda Juventus mwaka 2012 kabla ya kiungo huyo hajapata nafasi ya kucheza katika kikosi cha kwanza cha Sir Alex Ferguson. Lakini Pogba amekwenda jijini Turin na kuimarika na kwa mmoja katia ya wachezaji duniani, akiisaidia Juventus kutwaa mataji manne mfululizo ya Serie A huku pia akiisaidia nchi yake katika kipindi cha miaka minne iliyopita. United wamepania kumrejesha Pogba Old Trafford lakini wameshaambiwa na Juventus kuwa anaweza kuwagharimu ada ya paundi milioni 100 ambayo itavunja rekodi ya usajili duniani. Mazungumzo pia yanaendelea kati ya Zlatan Ibrahimovic ambaye ni mchezaji huru kufuatia nchi yake kutolewa katika michuano ya Ulaya inayoendelea nchini Ufaransa na kuamua kustaafu soka la kimataifa.

No comments:

Post a Comment