Monday, June 27, 2016

RASMI BLANC AONDOKA PSG.

KLABU ya Paris Saint-Germain-PSG imetangaza rasmi kuwa Laurent Blanc ameondoka katika timu hiyo kwa maelewano. Mapema mwezi huu kuna taarifa zilizagaa kuwa Blanc alitarajiwa kutimuliwa na nafasi yake kuchukuliwa na Unai Emery, meneja wa zamani wa Sevilla ambaye ameshinda mataji matatu mfululizo ya Europa League. PSG sasa wamethibitisha taarifa hizo za kuachana na Blanc ambaye ameiwezesha timu hiyo kutwaa mataji matatu ya nyumbani katika msimu miwili iliyopita lakini amekuwa akikwama katika hatua ya robo fainali ya michuano ya Ligi ya Mabingwa ulaya katika misimu mitatu aliyoinoa klabu hiyo. Katika taarifa ya klabu hiyo iliyotumwa katika mtandao wake imedai kuwa wameachana na Blanc baada ya kufikia makubaliano kwa faida ya pande zote mbili. Taarifa hiyo iliendelea kudai kuwa kocha msaidizi Jean-Louis Gasset na mwalimu wa mazoezi Philippe Lambert nao pia wataondoka wakati klabu hiyo ikijaribu kuajiri benchi jipya kabisa la ufundi.

No comments:

Post a Comment