Monday, June 27, 2016

BRAVO ANA MATUMAINI MESSI ATABADILI UAMUZI WAKE.

KIPA wa mabingwa wa Copa America Chile, Claudio Bravo ana matumaini mchezaji mwenzake wa Barcelona Lionel Messi atafikiria tena uamuzi wa kustaafu soka la kimataifa na kuendelea kuitumikia Argentina. Messi akiwa katika huzuni aliushtusha ulimwengu baada ya Argentina kushindwa kwa changamoto ya mikwaju ya penati kwa Chile katika fainali ya Copa America mapema leo, kutangaza kustaafu kuitumikia nchi yake. Nyota huyo ambaye ndio mfungaji bora wa wakati wote wan chi hiyo, alikuwa akibubujikwa na machozi kufuatia kukosa penati ambapo ilipelekea Argentina kupata kipigo cha tatu katika fainali za michuano mikubwa. Akihojiwa Bravo amesema kwake Messi ni mchezaji bora duniani na wote wanafahamu ubora wake hivyo ni matumaini atabadili uamuzi wake na kuendelea kuitumikia Argentina.

No comments:

Post a Comment