Monday, June 27, 2016

COPA AMERICA 2016: SANCHEZ ATWAA GOLDEN BALL WAKATI CHILE WAKIKWANGUA TUZO ZOTE.

MSHAMBULIAJI nyota wa Arsenal, Alexis Sanchez ametajwa kuwa mchezaji bora wa mashindano wakati mabingwa wa Copa America Chile wakichukua tuzo zote za mchezaji mmoja mmoja. Chile waliichapa Argentina kwa changamoto ya mikwaju ya penati kwa mwaka wa pili mfululizo katika fainali iliyofanyika mapema leo na Sachez akitwaa tuzo ya Mpira wa Dhahabu kama mchezaji bora baada ya kufunga mabao matatu na kusaidia mengine mawili katika mechi sita. 
Mchezaji mwenzake wa Chile Eduardo Vargas alitwaa tuzo ya Kiatu cha Dhahabu baada ya kumaliza kinara wa mabao akiwa na mabao sita huku kipa Claudio Bravo yeye akishinda Golden Cloves kwa kuruhusu nyavu zake kutikiswa mara moja pekee katika michuano hiyo. Chile ndio waliotawala katika kikosi bora cha michuano hiyo baada ya wachezaji nane kuteuliwa, pamoja na wengine watatu wa Argentina akiwemo Lionel Messi ambaye alikosa penati katika mchezo huo.

No comments:

Post a Comment