Monday, June 27, 2016

DONE DEAL: SAIDO MANE TO LIVERPOOL.

MSHAMBULIAJI wa Southampton, Sadio Mane anatarajiwa kufanyiwa vipimo vya afya leo Liverpool baada ya klabu hizo kukubaliano ada ya uhamisho wake ambayo inakadiriwa kufikia kiasi cha paundi milioni 30. Kama dili hilo likikamilika, itakuwa moja ya usajili ghali Liverpool ukishindana na ule wa paundi milioni 32.5 zilizolipwa kwa ajili ya Christian Benteke na paundi milioni 35 kwa ajili ya Andy Carroll. Meneja wa Liverpool Jurgen Klopp anataka kuimarisha safu yake ya ushambuliaji na alimpa Mane kipaumbele katika usajili wa kipindi hiki cha kiangazi. Klopp alivutiwa na Mane wakati alipowafunga mara mbili wakati Southampton walipotoka nyuma kwa mabao 2-0 na kuja kuifunga Liverpool mabao 3-2 katika Uwanja wa St Mary’s Machi 20 mwaka huu. Mane sasa anaungana na mshambuliaji nyota wa kimataifa wa Uingereza Daniel Sturridge na chipukizi wa Ubelgiji Divock Origi ambaye alifunga mabao 11 katika mechi 37 msimu uliopita.

No comments:

Post a Comment