Monday, June 27, 2016

ALMOST DONE DEAL: DANI ALVES TO JUVENTUS.

BEKI wa Barcelona, Dani Alves anatarajiwa kukamilisha uhamisho wake kwenda kwa mabingwa wa Serie A Juventus baada ya kusafiri jana jioni kuelekea jijini Turin. Alves alithibitisha mwanzoni mwa mwezi huu kuwa atajiunga na Juventus baada ya kukaa Barcelona kwa misimu nane na sasa uhamisho huo unaonekana kukaribia kukamilika. Nyota huyo mwenye umri wa miaka 33 bado ana mkataba wa mwaka mmoja na Barcelona lakini klabu hiyo imekubali kumruhusu kuhama akiwa kama mchezaji huru. Juventus walituma picha na video ya mchezaji huyo katika ukurasa wao wa mtandao wa kijamii wa twitter wakionyesha akitua jijini Turin. Juventus imefanikiwa kutwaa taji la tano la Serie A msimu uliopita pamoja na kuondoka kwa nyota wake kadhaa akiwemo Andra Pirlo, Arturo Vidal na carlos Tevez ambao wlaiisaidia timu hiyo kutinga fainali ya michuano ya Ligi ya Mabingwa mwaka 2014 na kuja kupoteza kwa kufungwa na Barcelona mabao 3-1.

No comments:

Post a Comment