Thursday, June 30, 2016

MANC CITY YAKAMILISHA USAJILI WA MOOY.

KLABU ya Manchester City imekamilisha usajili wa nyota wa kimataifa wa Australia Aaron Mooy kutoka Meolbourne City klabu ambayo pia wanaimiliki. Uhamisho huo ulithibitishwa jana ambapo nyota huyo sasa anahamia City kwa mkataba wa miaka mitatu. Mooy mwenye umri wa miaka 25 amekuwa akitwaa tuzo ya mchezaji wa mwaka katika klabu hiyo toka alipojiunga nao akitokea kwa mahasimu wao Western Sidney Wanderers mwaka 2014. Hata hivyo, Mooy anatarajiwa kupelekwa kwa mkopo kwanza pindi atakapotua Manchester.

No comments:

Post a Comment