Thursday, June 30, 2016

MADRID YAMTENGEA ALABA EURO MILIONI 65.

KLABU ya Real Madrid inadaiwa kutoa ofa ya euro milioni 65 kwa ajili ya kumuwania nyota wa Bayern Munich David Alaba. Wakongwe hao wa soka wa Hispania wameamua kumuwinda kwa udi na uvumba nyota huyo wa kimataifa wa Austria kiangazi hiki na sasa wameboresha ofa yao kutoka euro milioni 50 walizotoa mara ya kwanza. Ingawa Bayern hawajatamka lolote kuhusu ofa hiyo, inafahamika kuwa wanataka euro milioni 80 kwa timu itakayomuhitaji Alaba. Mbali na Alaba, Madrid pia wameonyesha nia ya kutaka kumsajili kiungo wa mabingw awa Ligi Kuu Leicester City N’golo Kante.

No comments:

Post a Comment