Thursday, June 30, 2016

SIMEONE ASISITIZA KUENDELEA KUBAKIA ATLETICO.

MENEJA wa Atletico Madrid, Diego Simeone amefafanua kauli yake aliyoitoa kufuatia timu yake kupoteza mchezo wa fainali ya Ligi ya Mabingwa Ulaya mwezi uliopita. Atletico ilishindwa kutamba kwa mara ya pili katika kipindi cha miaka mitatu baada ya kutandikwa tena mahasimu wao wa jiji Real Madrid. Baada ya mchezo huo ambao walipoteza kwa changamoto ya mikwaju ya penati jijini Milan, Simeone amesema anatarajiwa kuchukua muda kufikiria kuhusu mustakabali wake katika klabu hiyo. Lakini meneja huyo mwenye umri wa miaka 46 amesema kauli hiyo aliitoa wakati akiwa katika kipindi kibaya, kwani hana mpango wowote wa kuondoka Atletico kwasasa. Simeone aliendelea kudai kuwa Atletico itaendelea kuwa moja ya vikosi bora kabisa katika ulimwengu wa soka katika miaka mingi ijayo. Meneja huyo amesema timu pekee zinazowazidi kwa ubora ni Barcelona, Real Madrid na Bayern Munich, hakuna nyingine.

No comments:

Post a Comment