Thursday, June 30, 2016

NOLITO ANUKIA CITY.

WINGA mahiri wa kimataifa wa Hispania, Nolito anadaiwa kuwa tayari ameshatua jijini Manchester kwa ajili ya kukamilisha uhamisho wake kwenda Manchester City. Nyota huyo anatarajiwa kuwa mchezaji wa pili kusajili na meneja mpya wa klabu hiyo Pep Guardiola baada ya kufikia makubaliano mabo binafsi na timu hiyo ya Ligi Kuu. Nolito anatarajiwa kumalizia baadhi vitu vichache vilivyobaki katika uhamisho wake kutoka Celta Vigo ambao umegharimu kiasi cha paundi milioni 14, pindi atakapotembelea kituo cha michezo cha City. Mara baada ya kukamilisha vipimo vyake vya afya, Nolito anatarajiwa kutembezwa katika kituo hicho kabla ya kupigwa picha na kutambulishwa rasmi kwa vyombo vya habari. Nyota huyo atakuwa mchzaji pili kusajiliwa na City baada ya Ilkay Gundogan aliyesajiliwa kutokea Borussia Dortmund Juni 2 mwaka huu.

No comments:

Post a Comment