Thursday, June 30, 2016

SCOLARI ATAMANI KUINOA UINGEREZA.

KOCHA wa zamani wa Brazil, Luiz Felipe Scolari ametangaza nia yake ya kuja kuwa meneja ajaye wa timu ya taifa ya Uingereza. Kocha huyo mwenye umri wa miaka 67 ambaye aliiongoza Brazil kutwaa Kombe la Dunia mwaka 2002, alipata nafasi ya kuchukua mikoba ya Sven-Goran Eriksson kama meneja wa Uingereza mwaka 2006 kabla ya kujitoa kutokana na kushambuliwa na vyombo vya habari vya nchi hiyo. Scolari ambaye alishindwa kupata mafanikio katika klabu ya Chelsea kwa kutimuliwa baada ya miezi sita, amesisitiza kuwa yuko tayari kwa chochote ambacho Chama cha Soka Uingereza kitahitaji kutoka kwake kama akiteuliwa kuwa kocha. Akihojiwa Scolari amesema kwasasa yeye bado ni meneja wa Guanghou na anakipenda kibarua chake lakini anafahamu umuhimu wa kibarua cha kuinoa Uingereza katika ulimwengu wa soka hivi sasa. Kocha huyo aliendelea kudai kuwa anahusudu soka la Uingereza na anafahamu mahitaji ya timu ya taifa kuwa inahitaji mafanikio.

No comments:

Post a Comment