Thursday, June 30, 2016

HULK AKAMILISHA USAJILI WAKE CHINA.

KLABU ya Shanghai SIPG imekamilisha rasmi usajili wa nyota wa kimataifa wa Brazil, Hulk kutoka klabu ya Zenit St Petersburg ya Urusi. Klabu hiyo inayoshiriki Ligi Kuu ya China-CLS imelipa kitita cha euro milioni 56 kwa mchezaji huyo ambachi kimeweka rekodi mpya ya usajili katika ligi hiyo. Zenit pia wanatarajiwa kupata bakshishi ya euro milioni mbili zaidi kama mshambuliaji huyo atafunga mabao zaidi ya 15. Inadaiwa kuwa Hulk amekubalia mshahara wa euro milioni 12.5 kabla ya bakshishi, kiasi ambacho kitamfanya kuwa mchezaji anayelipwa zaidi CLS. Klabu hiyo ilithibitisha taarifa hizo kupitia mtandao wake na kudai kuwa Hulk alisaini mkataba wake pindi alipomaliza vipimo vyake vya afya.

No comments:

Post a Comment