Thursday, June 30, 2016

CHILE KUCHEZA NA MABINGWA WA EURO 2016.

MABINGWA wa michuano ya Copa America, Chile wanatarajiwa kupambana na bingwa wa michuano ya Ulaya anakayepatikana baadae mwezi ujao. Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa na rais wa Shirikisho la Soka la America Kusini-CONMEBOL, Alejandro Dominguez, mchezo huo utakaokutanisha bingwa wa Copa America na Euro 2016 utachezwa katika miezi michache ijayo. Wakati Chile wakijihakikishia nafasi yao ya kushiriki Kombe la Shirikisho mwaka 2017, Dominguez amebainisha kuwa tayari wameshatuma barua ya maombi ya mchezo huo kwa Shirikisho la Soka la Ulaya. Dominguez amesema mara baada ya kutuma barua hiyo wamepata majibu ya matumaini kwamba mchezo huo unaweza kuwepo hivyo wanachotakiwa kufanya ni kutafuta tarehe itakayofaa.

No comments:

Post a Comment