Thursday, June 30, 2016

WENGER ADAIWA KUWA TAYARI KUINOA UINGEREZA.

VYOMBO vya habari nchini Uingereza vimeripoti kuwa meneja wa Arsenal, Arsene Wenger yuko tayari kujadili kibarua cha kuinoa timu ya taifa ya nchi hiyo wakati mkataba wake utakapomalizika mwaka ujao. Wenger mwenye umri wa miaka 66, amekuwa akitajwa kama mmoja wa makocha wanaoweza kuchukua ya kuinoa Uingereza iliyoachwa wazi na Roy Hodgson, lakini kocha huyo amekuwa akisisitiza anataka kumaliza mkataba wake na Arsenal kabla ya kufanya maamuzi yeyote. Uingereza kwasasa haina kocha baada ya Hodgson kuondoka kufuatia kutolewa katika michuano ya Ulaya na Iceland lakini ofisa mkuu wa FA Martin Glenn amesema yuko tayari kusubiri mpaka watakapopata mtu wanayemuhitaji, huku magazeti ya The Times na Telegraph yakidai kuwa Wenger atakuwa tayari kwa kibarua hicho. Kama Mfaransa huyo atakuwa tayari, hata hivyo dili lolote kwa ajili ya kuchukua kibaua hicho itabidi lifanyike kiangazi mwakani hivyo FA italazimika kutafuta kocha wa muda katika kampeni zao za kufuzu Kombe la Dunia. Gareth Southgate ambaye anakinoa kikosi cha vijana wa chini ya umri wa miaka 21 wa nchi hiyo, amekuwa akitajwa kupewa kibarua cha muda kufundisha kikosi cha wakubwa wakati wakitafuta mbadala wa Hodgson.

No comments:

Post a Comment