Wednesday, June 22, 2016

NOLITO ANUKIA MAN CITY.

KLABU ya Manchester City, inadaiwa kukaribia kumsajili mshambuliaji wa kimataifa wa Hispania, Nolito kutoka Celta Vigo. Nyota huyo mwenye umri wa miaka 29 amethaminishwa kwa kiasi cha euro milioni 18 katika mkataba wake, na rais wa Celta Vigo Carlos Mourino tayari ameshadokeza kuwa anategemea ataondoka kiangazi hiki. Taarifa zilizotolewa na gazeti la Gurdian la Uingereza zimedai kuwa City wana uhakika wa kukamilisha dili hilo na kuongeza kuwa Nolito tayari ameshakubali mambo binafsi katika mkataba wa miaka mitatu atakaopewa wenye thamani ya euro milioni nne kila msimu. Mchezaji huyo wa zamani wa Barcelona, ambaye amecheza katika mechi zote tatu za Hispania katika michuano ya Ulaya inayoendelea nchini Ufaransa, amekuwa pia akihusishwa na tetesi za kurejea Camp Nou. Nolito ambaye atafikisha miaka 30 Octoba mwaka huu, aliondoka Barcelona na kwenda Benfica mwaka 2011 kabla ya kujiunga na Celta Vigo miaka miwili baadae.

No comments:

Post a Comment