Wednesday, June 22, 2016

MADRID YATHIBITISHA KUMREJESHA MORATA.

KLABU ya Real Madrid imethibitisha kuwa Alvaro Morata atarejea Santiago Bernabeu kipindi hiki cha kiangazi. Taarifa hizo zimekuwa mapema baada ya mkurugenzi mtendaji wa Juventus Beppe Marotta kubainisha kuwa Morata anategemewa kurejea Madrid. Madrid walikuwa na nafasi ya upendeleo ya kumnunua tena Morata mwenye umri wa miaka 23, ikiwa ni sehemu ya mkataba uliopelekea nyota huyo wa kimataifa wa Hispania kujiunga na Juventus miaka miwili iliyopita na sasa wamethibitisha kufanya hivyo. Katika taarifa yao iliyotumwa katika mtandao, Madrid walithibitisha taarifa hiyo na kudai kuwa Morata atajiunga na mazoezi ya maandalizi ya msimu mpya wa La Liga chini ya meneja Zinedine Zidane. Hata hivyo, taarifa zinadai kuwa Madrid wanaweza kumuuza Morata kwa klabu nyingine ili wapate faida.

No comments:

Post a Comment