Wednesday, June 22, 2016

CHELSEA YAPANIA KUNASA SAINI YA BEKI WA NAPOLI.

KLABU ya Chelsea inadaiwa kuanza kumuwania beki wa Napoli Kalidou Koulibaly kwa kutoa ofa ya paundi milioni 19.2. Chelsea wamekuwa wakimhusudu kwa kiasi kikubwa beki huyo wa kimataifa wa Senegal, ambaye ameingia katika mzozo na klabu yake kuhusiana na uhamisho wake. Hata hivyo, ofa hiyo ya Chelsea tayari imeshakataliwa na Napoli wamedai wanataka kitita cha paundi milioni 30 ili waweze kumuachia nyota huyo mwenye umri wa miaka 24. Napoli walichukizwa na Koulibaly kufuatia madai aliyotoa kuwa yuko tayari kuzungumza na Chelsea. Beki huyo amesema hajazungumza na Antonio Conte lakini anadhani hilo litafanyika hivi karibuni.

No comments:

Post a Comment