Wednesday, June 22, 2016

PAUL CLEMENT KUWA MSAIDIZI WA ANCELOTTI BAYERN.

KLABU ya Bayern Munich, imemteua Paul Clement kuwa meneja msaidizi wa timu hiyo. Kocha huyo mwenye umri wa miaka 44 ataungana bosi wake wa zamani Muitaliano Carlo Ancelotti katika benchi la ufundi la klabu hiyo, wakiwa wameshawahi kufanya kazi pamoja katika klabu za Chelsea, Paris Saint-Germain na Real Madrid. Clement aliteuliwa kuwa kocha wa Derby Count Juni mwaka 2015 kufuatia Ancelotti kutimuliwa Madrid lakini alitimuliwa na timu hiyo Februari mwaka huu wakati wakishika nafasi ya tano katika Ligi ya Ubingwa. Kocha huyo Muingerza ataanza kufanya kazi pindi mabingwa hao wa Bundesliga na Kombe la Ujerumani watakaporejea katika mazoezi ya maandalizi ya msimu mpya katika kipindi cha wiki tatu zijazo.

No comments:

Post a Comment