Wednesday, June 22, 2016

CHAMPIONSHIP 2016-2017: DI MATTEO KUANZA NA DERBY YA BIRMINGHAM, BENITEZ KUKWAANA NA FULHAM.

KLABU ya Newcastle United chini ya Rafa Benitez inatarajiwa kuanza maisha mapya katika Ligi ya Ubingwa kwa kusafiri kuifuata Fulham katika mchezo wa ufunguzi wa ligi hiyo msimu wa 2016-2017. Newcastle wanataka kurejea haraka katika Ligi Kuu kufuatia kushushwa kutoka huko msimu uliopita. Mchezaji wa kwanza wa Newcastle watakaochezwa nyumbani katika ligi hiyo utakuwa dhidi ya Huddersfield Town Agosti 13 mwaka huu. Nayo Aston Villa mchezo wa kwanza toka washushwe daraja utakuwa dhidi ya Sheffield Wadnesday huko Hillsborough. Villa ambao watakuwa chini ya meneja wao mpya Roberto Di Matteo watavaana na Birmingham ambao ni mahasimu wao kutoka mji mmoja Octoba 29 mwaka huu huko St.Andrews huku marudiano yakitarajiwa kuwa Aprili 22 mwakani. Norwich City, ambao walijiunga na Newcastle na Villa katika timu zilizoshuka daraja msimu uliopita, wao wataanza kampeni zao kwa kupambana na Blackburn Rovers.

No comments:

Post a Comment