Friday, July 22, 2016

BAADA YA GOTZE, DORTMUND SASA YAMNASA SCHURRLE.

KLABU ya Borussia Dortmund imetangaza kumsajili rasmi Andre Schurrle kutoka Wolfsburg ya Ujerumani. Nyota huyo wa zamani wa Chelsea amesaini mkataba wa miaka mitano na Dortmund akijiunga nao siku moja baada ya kumsajili Mario Gotze. Akihojiwa na mtandao wa klabu hiyo, Schurrle amesema Dortmund ni moja kati ya klabu kubwa Ulaya huku wakiwa na kikosi imara na kinachovutia. Schurrle aliendelea kudai kuwa ana matumaini makubwa ya kufanya vizuri akiwa na Dortmund na kuwaomba mashabiki wamuunge mkono ili aweze kusaidia kuleta mataji.

No comments:

Post a Comment