Friday, July 22, 2016

WAKALA WA POGBA ADAI ANAJALI ZAIDI MASLAHI YA MTEJA WAKE KULIKO REKODI.

WAKALA wa Paul Pogba, Mino Raiola amesema hajali sana kama Manchester United watatoa ada itakayovunja rekodi kwa ajili ya kumnasa mteja wake kutoka Juventus na kusisitiza anachojali yeye ni mkataba mnono atakaoupata. Nyota huyo wa kimataifa wa Ufaransa aliondoka Old Trafford kwenda kujiunga na Juventus akiwa mchezaji huru mwaka 2012 na toka wakati huo ameimarika na kuwa mmoja wa wachezaji bora duniani akishinda mataji manne mfululizo ya Serie A. Taarifa zinadai kuwa Pogba mwenye umri wa miaka 23 anakaribia kujiunga na United kwa kitita cha euro milioni 110, wakati taarifa zingine zikidai Raiola anaweza kukunja kiasi cha euro milioni 21 katika dili yeyote itakayofanikiwa. Kama akisajili wa kiasi hicho, atakuwa ameipita rekodi ya dunia ya usajili ya euro milioni 100 ambazo Real Madrid walilipa kwa ajili ya kumsajili Gareth Bale kutoka Tottenham hotspurs. Hata hivyo, Raiola amesema ada ya uhamisho wa Pogba sio vitu vinavyomtia shaka kwasasa kwani yeye anachijali zaidi ni mteja wake kupata mkataba mnono.

No comments:

Post a Comment