Friday, July 22, 2016

DAKTARI BINGWA WA MIFUPA AMUONDOA HOFU BA.

Daktari wa upasuaji wa Demba Ba, Olivier Bringer amewasili jijini Shanghai na kubainisha kuwa ana uhakika mshambuliaji huyo wa zamani wa Chelsea ataweza kurejea tena uwanjani na kucheza soka la ushindani. Daktari huo mtaalamu wa masuala ya mifupa kutoka Ufaransa, alitua jijini humo jana na moja kwa moja alikwenda katika hospitali ya Putuo ambako nyota huyo wa kimataifa wa Senegal amelazwa toka alipovunjika vibaya mguu wake wa kushoto wakati akiichezea timu yake ya Shenghua Jumapili iliyopita. Bringer amesema ana uhakika Ba ataweza kupona na kurejea kucheza soka tena baada ya miezi michache. Ba anatarajiwa kufanyiwa vipimo vingine kesho wakati timu ya madaktari waliokuja na Bringer itakapopewa maendeleo ya nyota huyo na madaktari wa hospitali hiyo aliyolazwa.

No comments:

Post a Comment