Friday, July 22, 2016

BARCELONA YAKUBALI KUMSAJILI GOMES.

KLABU ya Barcelona imetangaza kufikia makubaliano na Valencia ya kumsajili kiungo wa kimataifa wa Ureno Andre Gomes. Gomes ameitumikia Valencia kwa misimu miwili baada ya kuhamia hapo akitokea Benfica Julai mwaka 2014. Nyota huyo mwenye umri wa miaka 22, alikuwa sehemu ya kikosi cha timu ya taifa ya Ureno kilichotwaa taji la michuano ya Ulaya mwaka huu. Taarifa zinadai kuwa Barcelona imelipa kiasi cha euro milioni 40 kwa ajili ya kupata saini ya Gomes ambaye amecheza mechi 30 na kufunga mabao matatu msimu uliopita. Usajili wake ukikamilika atakuwa mchezaji wa nne kusajiliwa na Barcelona baada ya Samuel Umtiti, Lucas Digne na Denis Suarez.

No comments:

Post a Comment