Friday, July 22, 2016

LONG AJITIA KITANZI SOUTHAMPTON.

MSHAMBULIAJI wa Southampton, Shane Long amejitia kitanzi kwa kusaini mkataba mpya wa miaka minne na klabu hiyo. Long ambaye alihamia Southampton akitokea Hull City miaka miwili iliyopita, anatarajiwa kuendelea kuitumikia klabu hiyo mpaka mwaka 2020. Nyota huyo wa kimataifa wa Jamhuri ya Ireland, amefunga mabao 21 katika misimu miwili ambayo amecheza Southampton. Akihojiwa Long amesema kikubwa kilichomsukuma kusaini mkataba huo ni mashabiki wa klabu ambao siku zote wamemfanya ajisikie yuko nyumbani. Long anatarajiwa kufanya kazi chini ya meneja mpya wa Southampton baada ya kocha wa zamani wa Lyon na Nice Claude Puel kuchukua nafasi ya Ronaldo Koeman ambaye amekwenda kuinoa Everton.

No comments:

Post a Comment