Thursday, July 21, 2016

HISPANIA YAPATA KOCHA MPYA BAADA YA DEL BOSQUE KUONDOKA.

SHIRIKISHO la Soka la Hispania, limemteua Julian Lopetegui kuwa kocha mpya wa timu ya taifa ya nchi hiyo akichukua nafasi ya Vicente del Bosque. Del Bosque alijiuzulu wadhifa wake huo kufuatia kutofanya vyema katika michuano ya Ulaya mwaka huu na sasa Lopetegui, meneja wa zamani wa FC Porto ndiye atakayeiongoza nchi hiyo kuelekea katika michuano ya Kombe la Dunia mwaka 2018. Lopetegui amewahi kuviongoza vikosi cha timu ya taifa ya Hispania kwa vijana chini ya umri wa 19, 20 na 21, huku akishinda taji la michuano ya Ulaya akiwa na vikosi vya vijana chini ya umri wa miaka 19 na 21. Kocha huyo pia amewahi kuiongoza Porto kwa misimu miwili huku akimaliza katika nafasi ya pili msimu wa 2014-2015 na tatu msimu uliofuata kabla ya kutimuliwa Januari mwaka huu na nafasi yake kuchukuliwa na Rui Barros. Lopetegui mwenye umri wa miaka 49, ambaye aliwahi kucheza katika klabu za Real Madrid na Barcelona akiwa kipa, kibarua chake cha kwanza kitakuwa mwezi ujao wakati watakapochuana na Ubelgiji katika mchezo wa kimataifa wa kirafiki.

No comments:

Post a Comment