Thursday, July 21, 2016

RASMI: GOTZE AREJEA DORTMUND.

KLABU ya Borussia Dortmund imetangaza kumsajili tena kiungo Mario Gotze kutoka kwa mahasimu wao wa Bundesliga Bayern Munich. Katika taarifa yake waliyoitoa katika mtandao wao, Dortmund wamekubali kumsajili tena kiungo kwa mkataba utakaomalizika mwaka 2020 na anatarajiwa kukamilisha uhsmaisho huo baada ya kufaulu vipimo vya afya. Nyota huyo wa kimataifa wa Ujerumani mwenye umri wa miaka 24, ambaye mkataba wake unamalizika msimu ujao, alishindw akung’aa toka atue Allianz Arena mwaka 2013 kutokana na kusumbuliwa na majeruhi ya mara kwa mara. Bayern nao walithibitisha suala hilo katika mtandao wao na kumshukuru Gotze kwa mchango wake katika kipindi chote cha miaka mitatu waliyokuwa naye.

No comments:

Post a Comment