Monday, July 25, 2016

HALI MBAYA YA HEWA YAPELEKEA MCHEZO WA UNITED NA CITY KUFUTWA HUKO CHINA.

MECHI ya kirafiki kati ya miamba wa Uingereza, Manchester City na Manchester United, imefutwa kutokana na hali mbaya ya hewa. Mchezo huo uliokuwa umepangwa kuchezwa katika Uwanja wa Bird Nest uliopo jijini Beijing, China ungekuwa wa kwanza kuzikutanisha timu hizo wakiwa na mameneja wao wapya Pep Guardiola na Jose Mourinho. Jana, Mourinho alikuwa amedokeza kwamba hali katika uwanja huo ilikuwa mbaya. Hata kabla ya mechi kuahirishwa rasmi, Guardiola alikuwa amesema matumaini yake ni kwamba wachezaji wake wasiumie. Klabu zote mbili zimeafiki kwa pamoja kuahirisha mchezo huo huku United wakitarajiwa kurejea Uingereza leo na City wao watasafiri kwenda Shenzhen kesho kwa ajili ya kwenda kucheza na Borussia Dortmund ya Ujerumani Alhamisi. Mvua kubwa ilinyesha Jumapili na watabiri wa hali ya hewa walisema mvua zaidi ingenyesha Jumatatu.

No comments:

Post a Comment