Monday, July 25, 2016

ALLARDYCE AKATAA KUMUHAKIKISHIA ROONEY UNAHODHA.

KOCHA wa timu ya taifa ya Uingereza, Sam Allardyce amesema kibarua chake kipya kitakuwa na changamoto kubwa katika maisha yake ya soka. Akizungumza na wanahabari kwa mara ya kwanza toka ateuliwe kushikilia wadhifa huo, Alladyce amesema hazina yake kubwa ni suala la utawala. Allardyce ambaye aliisaidia Sunderland isishuke daraja msimu uliopita, amechukua nafasi ya Roy Hodgson aliyeondoka baada ya kutofanya vyema katika michuano ya Ulaya iliyofanyika nchini Ufaransa mwaka huu. Sammy Lee aliyekuwa msaidizi wa Allardyce wakati akiinoa Bolton Wanderers, naye ataungana katika benchi ya ufundi la Uingereza. Allardyce amesema anafahamu kuwa kibarua hicho kitakuwa na changamoto kubwa katika maisha yake ya soka lakini ana matumaini atapata mafanikio kama ilivyo huko nyuma. Kocha huyo pia amesema hatafanya uamuzi wowote kuhusu unahodha wa Wayne Rooney mpaka atakapokutana na wachezaji na viongozi wengine.

No comments:

Post a Comment