Monday, July 25, 2016

AUBAMEYANG AIRAHISISHIA KAZI MADRID.

MSHAMBULIAJI nyota wa Borussia Dortmund, Pierre-Emerick Aubameyang amedai kuwa kuichezea Real Madrid ni moja ya malengo yake makubwa na mabingwa hao wa Ulaya ndio klabu pekee inaweza kumshawishi kuondoka Ujerumani. Mapema mwaka huu katika mahojiano nyota huyo wa kimataifa wa Gabon alidai kumuahidi babu yake kuwa siku moja atakuja kuichezea Madrid. Taarifa zimekuwa zikizagaa kuwa mshambuliaji huyo aliyefunga mabao 39 akiwa na Dortmund msimu uliopita, amekuwa akiwaniwa kwa fedha nyingi na klabu za Manchester City na Atletico Madrid kiangazi hiki. Lakini mwenyewe sasa ameweka wazi kuwa ni Zinedine Zidane pekee anayeweza kumng’oa kutoka Signal Iduna Park. Akihojiwa Aubameyang amesema kwa mwaka huu uhamisho hautawezekana lakini klabu pekee anayoweza kwenda badala ya Dortmund ni Madrid na kama hawatakuja kumuwania basi hana mpango wa kwenda popote.

No comments:

Post a Comment