Monday, July 25, 2016

ALLEGRI AGOMA KUZUNGUMZIA KUONDOKA KWA POGBA NA UJIO WA HIGUAIN.

MENEJA wa Juventus, Massimiliano Allegri amesema klabu inafanya vizuri na shughuli za usajili kiangazi hiki lakini amekataa kuzungumzia mustakabali wa Paul Pogba anayewindwa na Manchester United au suala la ujio wa mshambuliaji wa Napoli Gonzalo Higuain. Leo, vyombo vya habari nchini Uingereza vimeripoti kuwa United wameongeza ofa yao ya paundi milioni 92 kwa kuongeza paundi milioni 10 ili waweze kumnasa kiungo huyo kwa usajili utakaovunja rekodi ya dunia. Hata hivyo, Allegri alikataa kutoa kauli yeyote kuhusiana na suala hilo pamoja na zile taarifa za Juventus kukaribia kukamilisha usajili wa Higuain utakaowagharimu kiasi cha euro milioni 97.4. Akizungumza na wanahabari jijini Melbourne kuelekea mchezo wao wa kirafiki wa michuano ya kimataifa dhidi ya Tottenham Hotspurs kesho, Allegri amesema hatazungumza masuala ya usajili kwani wapo hapo kwa ajili ya maandalizi ya mchezo wao dhidi ya Spurs.

No comments:

Post a Comment