Monday, July 25, 2016

POCHETTINO ACHOMOA KUINOA ARGENTINA.

MENEJA Mauricio Pochettino amejitoa kufuatia tetesi kuwa anaweza kuchukua nafasi ya Gerardo Martino kama kocha wa mpya wa Argentina, na kudai kuwa huu sio wakati muafaka wa kuondoka Tottenham Hotspurs. Pochettino mwenye umri wa miaka 44, ni moja kati ya majina yaliyotajwa kuhusishwa na kibarua hicho kufuatia kujiuzulu kwa Martino baada ya Argentina kufungwa tena na Chile katika fainali ya michuano ya Copa America. Lakini Pochettino ambaye amesaini mkataba mpya wa miaka mitano na Spurs Mei mwaka huu, amesisitiza anafurahia kuendelea kuwepo White Hart Lane. Meneja huyo amesema anadhani tetesi ni suala la kawaida kwasababu yeye ni kocha raia wa Argentina ambaye anafundisha moja ya klabu kubwa nchini Uingereza. Lakini pamoja na tetesi hizo, Pochettinho aliendelea kudai kuwa kwasasa anafurahia kazi yake na kwasababu hiyo hadhani kama ni wakati muafaka kuikacha Spurs.

No comments:

Post a Comment